Translate

Tangazo la Hadithi

Thursday 26 December 2013

Tumetoka Mbali - Nelson Mandela




Nelson Mandela enzi za ujana wake



Nelson Mandela alikuwa ni Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini kutoka mwaka 1994 mpaka 1999. Bwana Nelson Mandela alizaliwa tarehe 18 July mwaka 1918; alifariki dunia tarehe 5 December mwaka 2013 akiwa na umri wa miaka 95  na kuzikwa kijijini kwake Qunu tarehe 15, December 2013. Nelson Mandela anajulikana sana kwa kupinga sera za ubaguzi wa rangi za Makaburu kulikopelekea afungwe jela kwa miaka 27. Nelson Mandela aliachiwa huru mwaka 1990.

Nelson Mandela alimuoa mke wake wa kwanza Evelyn Ntoko Mase tarehe 5 October 1944. Mandela na Evelyn walijaliwa kupata watoto wanne kwenye ndoa yao, ambao kati yao watatu wameshafariki na amebaki  mmoja anayeitwa Dr. Makaziwe Mandela ambaye anajulikana pia kama Maki. Mandela na Evelyn waliachana mwaka 1957 baada ya miaka  13 ya ndoa yao.

Nelson Mandela alimuoa mke wake wa pili, Winnie Madikizela-Mandela mwaka 1958. Mandela na Winnie walijaliwa kupata watoto 2, Zenani Mandela anayejulikana pia kama Zeni na Zindziswa Mandela-Hlongwane anayejulikana pia kama Zindzi. Nelson Mandela na Winnie Madikizela-Mandela walitengana mwezi April mwaka 1992 na waliachana kwa talaka mwezi March 1996.

Nelson Mandela alimuoa mke wake wa tatu bibi Graca Machel tarehe 18 July mwaka 1998 siku ya sherehe yake ya kutimiza miaka 80 ya kuzaliwa kwake.  




Nelson Mandela enzi za ujana wake





Nelson Mandela enzi za ujana wake






Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Bwana Nelson Mandela akiwa na mke wake wa kwanza Evelyn Ntoko Mase siku ya harusi yao mwaka 1944. Evelyn Mase na Nelson Mandela waliachana mwaka 1957.








Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Bwana Nelson Mandela akiwa na mke wake wa pili Winnie Madikizela Mandela siku ya harusi yao mwaka 1958. Winnie na Nelson Mandela walitengana mwaka 1992 na waliachana kwa talaka waka 1996.








Nelson Mandela na Winnie Madikizela-Mandela siku ya harusi yao mwaka 1958






Nelson Mandela na Winnie Madikizela-Mandela siku ya harusi yao mwaka 1958








Nelson Mandela na Winnie Madikizela-Mandela






Bwana Nelson Mandela akiwa na mke wake wa tatu, Bibi Graca Machel. Nelson Mandela na Graca Machel walioana siku ya sherehe za kumbukumbu ya miaka 80 ya kuzaliwa bwana Nelson Mandela mwaka 1998.






 Nelson Mandela akiwa na mke wake wa pili Winnie Madikizela Mandela mwaka 1990 siku chache baada ya kutoka gerezani





Nelson Mandela







Nelson Mandela





Bwana Nelson Mandela akiwa na aliyekuwa mke wake, Winnie Madikizela Mandela pamoja na baadhi ya wajukuu zao na vitukuu vyao.





Mabinti wa Nelson Mandela Dr. Makaziwe Mandela (kushoto), Zenani Mandela (katikati) na Zindziswa (Zindzi) Mandela (kulia)





Nelson Mandela akiwa na binti yake Zenani Mandela (kushoto) na mjukuu wake Ndileka Mandela (kulia)





Bwana Nelson Mandela akiwa na Binti yake Zenani Mandela, pamoja na watoto wa Zenani na wajukuu wa Zenani





Nelson Mandela akiwa na binti wake wa mwisho Zindziswa (Zindzi)





Nelson Mandela akiwa na Binti yake Dr. Makaziwe Mandela, mtoto wake kwa mke wake wa kwanza Evelyn Mase





Nelson Mandela akiwa na wajukuu zake



No comments:

Post a Comment